
Kwa upande wangu mimi nilishangaa TID kuhukumiwa kifungo, kwasababu siku ya tukio tulikuwa wote ukumbini, huyo dogo aliyemshitaki ndiye alikuwa na matatizo. Wiki hii tunakata rufaa, naamini siku chache zijazo TID atakuwa nje
*********@@@@@@@@@@*********
Mastaa hawa walivyoipokea hukumu ya TID
AY:
Ilinishutua sana, nimesikitika sana. Sikutegemea habari kama hiyo kwa kipindi hiki
Stara Thomas:
Du! Kwa kweli nilisikitika sana ila hakuna jinsi, kama kweli alipatikana na hatia atulie tu, hata familia yake pia itulie. Ni jambo linaloweza kumpata mtu yeyote, watulie tu mwaka utaisha atatoka, Mungu yupo. Ila sasa ni muda wa wasanii wote kuwa waangalifu sana na vitu tunavyofanya, maisha hayatabiriki.
Dudu:
Binafsi ilinishtua, ukizingatia kwamba nilikuwa sijui kama TID alikuwa na kesi. Ila nahisi TID alifanya uzembe kwa kudharau, kwasababu kesi kama hizi watu huwa wanamalizana kwa kuombana msamaha tu. Nasikitika kwasababu amefungwa kipindi hiki ambacho wasanii huwa tunatengeneza pesa sana, pia bendi yake, Top Band itakuwa katika wakati mgumu sana.
Prof J:
Ilinishtua sana, yaani kama naota, imeniuma lakini pia imenifundisha kuwasamehe wale wote niliokuwa na bifu nao. Nampa pole sana TID, kwasababu wote tuko chini ya sheria na tunaiheshimu.
Fid Q:
Niliipokea taarifa hiyo kwa masikitiko, lakini haijanishtua sana kwasababu nilitegemea kitu kama hicho. Kuna baadhi ya watu wana chuki na sisi wasanii, cha msingi ni kuwa makini ndiyo kitu nilichojifunza.
Madee:
Binafsi nahisi kama ni promosheni ambayo TID alikuwa anaitaka. Mtu kama yeye siyo wa kukosa laki mbili. Nauhakika mpaka wiki hii iishe TID atakuwa nje.
Mambo ya Flaviana MatataSauzi..
HII NDIYO NDOA YA JUMA NATURE!!